Wabaski

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sikukuu ya Artzaiak eta inudeak, Donostia, Ubaski.

Wabaski (kwa Kieuskara euskalduna) ni kabila la watu milioni 2-3 wanaoishi hasa Hispania kaskazini, lakini pia Ufaransa kusini-magharibi, mbali ya wengi waliohamia sehemu nyingine za dunia, hasa Amerika.

Lugha yao si kati ya lugha za Kihindi-Kiulaya.

Kati ya Wabaski maarufu zaidi, kuna mapadri watakatifu Ignas wa Loyola na Fransisko Saveri, waanzilishi wa Shirika la Yesu, na Mikaeli Garicoits, mwanzilishi wa Mapadri na mabradha wa Betharram.