Vicky Kamata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Vicky Paschal Kamata)
Vicky Paschal Kamata (Vicky Kamata Likwelile)
{{{maelezo_ya_picha}}}
{{{maelezo_ya_picha}}}
Afisa Uhusiano Taasisi ya Uhifadhi Wanyamapori Tanzania. (TAWA)
Bunge la 9 na 10
Jimbo la uchaguzi Geita
Tarehe ya kuzaliwa 18 Septemba 1978
Mahali pa kuzaliwa Tanga
Tarehe ya kifo
Chama chama cha mapinduzi (CCM)
Tar. ya kuingia bunge 2010
Alirudishwa mwaka
Aliondoka 2020
Alingia ofisini
Aliondoka ofisini
Alitanguliwa na
Alifuatwa na
Dini Mkristo
Elimu yake Shahada ya uzamili (Solent University UK)
Digrii anazoshika SAUT
Kazi
Mengine
Tovuti yake


Vicky Paschal Kamata (alizaliwa Tanga (mji), 18 Septemba 1978) ni mwanamuziki na mwanasiasa Mtanzania mwanachama wa chama cha kisiasa cha Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Alichaguliwa kuwa mbunge wa viti maalum kwa miaka 20102020. [1] Akiwakilisha wanawake wa mkoa wa Geita.

Pamoja na kuwa mwanamuziki mkongwe amekua akisaidia Jamii kupitia taasisi yake inayoitwa Victoria Foundation Archived 11 Aprili 2022 at the Wayback Machine. akiwa ni muanzilishi na Mkurugenzi wa taasisi hiyo iliyoanzishwa mwaka 2011.

Akiwa kama mwanamuzikk alitamba na nyimbo mbalimbalk na moja kati ya vibao vyake ambavyo hutamba mpaka sasa katika vituo mbalimbali vya Redio na Luninga ni wimbo wa wanawake na maendeleo ambao mpaka mwaka 2021 ulitimiza miaka 20.

Wimbo huo umekua ukitumika sana katika hafla mbalimbali zinazohusu wanawake na kuendeleza mijadala mizito yenye kuwapa nguvu wanawake duniani kote kujitambua na kuzijua haki zao katika kutafuta kipato.

Wimbo huo pia umemletea tuzo nyingi.


Vibao vingine alivyotamba navyo ni kama vile Sikumbuki Kuku, Fitina, Moyo wa Mtu kichaka, Mapenzi na Shule, Zingatia maadili, Nimeolewa nk.

Marejeo.[hariri | hariri chanzo]

  1. Tovuti ya Bunge la Tanzania, iliangaliwa Mei 2017