Vali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vali ya tairi: upepo unasukumwa ndani kwa shinikizo kubwa (P2) lakini hauwezi kutoka maana shinikizo la ndani (P1) linaifunga.

Vali au valvu (kutoka Kiingereza valve) ni kifaa kinachoruhusu kufungua, kufunga, kupunguza au kuongeza mwendo wa kimiminiko au gesi katika bomba au kifaa.

Kuna aina nyingi za valvu, zikiwa pamoja na

  • bilula (tapu ya maji, koki) kwenye mwisho wa bomba la maji
  • vali ya tairi inayoruhusu kuingiza upepo ndani yake na kuzuia hewa ya ndani isitoke
  • vali ya kudhibiti kumiminika kwa fueli katika injini au kutolewa kwa hewa chafu kutoka injini