Uwanja wa michezo wa Gelvandale

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Gelvandale Stadium ni uwanja wa michezo unaotumika kwa matumizi mbalimbali uliopo Port Elizabeth, Afrika Kusini.[1].Uwanja huo una njia ya mashindano ya mbio na hasa uwanja wa mpira wa miguu. Hivi sasa hutumiwa zaidi kama uwanja wa michezo wa jamii, na klabu ya mpira wa miguu ya ndani ya Swallows. Hivi sasa unatumiwa kama uwanja wa nyumbani wa muda wa Blackburn Rovers FC ya Afrika Kusini.[2]Uwanja huo hapo awali ulikuwa kutumiwa kwa mechi za mpira wa kulipwa ukiwa uwanja wa nyumbani wa klabu ya Daraja la Kwanza, Bay United F.C.. Baada ya kuhamishwa kwa Bay United, ilitumika kama uwanja wa nyumbani wa Bay Stars F.C. inayoshiriki ligi ya Daraja la Pili la SAFA.

Ulitumika pia kama uwanja wa mazoezi kwa timu zilizoshiriki katika Kombe la Dunia la FIFA mwaka 2010 na Kombe la Mataifa ya Afrika 2013, baada ya kujengwa na kufunguliwa Machi 2010[3]Iilikuwa moja ya nafasi mbili za Port Elizabeth zilizotumiwa na washiriki wa Kombe la Dunia kwa mazoezi yao na mechi za mazoezi kabla ya michezo yao katika uwanja wa Nelson Mandela Bay Stadium.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Port Elizabeth 2010 FIFA World Cup : Training Venues. Nelson Mandela Bay. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-04-13. Iliwekwa mnamo 2010-10-07.
  2. NMB, Gelvandale Stadium Amarova’s lucky charm. Zithethele (24 October 2013). Jalada kutoka ya awali juu ya 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 28 November 2013.
  3. Eastern Cape Development Corporation; newsroom; Nelson Mandela Bay on track with 2010 construction. Ecdc.co.za. Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-03-03. Iliwekwa mnamo 2010-10-07.
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu zaidi kuhusu Uwanja wa michezo wa Gelvandale kama historia yake, uenezi au kanuni zake?
Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.