Utendi wa Fumo Liyongo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Utendi wa Fumo Liyongo ni utenzi ulioandikwa na Muhamad Kijumwa ukiongelea mgogoro uliokuwepo kati ya Fumo Liyongo na kaka yake Daudi Mringwari. Utenzi huu uliandikwa mwaka 1913.

Katika utenzi huo, mtunzi anaanza kisa chake baada ya kuwa Fumo Liyongo [1] ameshakua na tayari anajulikana kama shujaa na mtu mwenye nguvu nyingi na uwezo wa kutunga na kukariri mashairi.

Utenzi huo unaonyesha jinsi Liyongo alivyokuwa shujaa wa vita katika kisiwa cha Pate katika karne ya 17, 18. Kama shujaa alipita changamoto, kulikuwa na njama za kumuua na kuepukaaa. Kwa sababu alikuwa shujaa sultani wa Pate alimuonea wivu.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Tenzi tatu za kale. Mulokozi, M. M. (Mugyabuso M.), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Dar es Salaaam: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. 1999. ISBN 9976-911-34-3. OCLC 45248518. 
Makala hii kuhusu kitabu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Utendi wa Fumo Liyongo kama Mwandishi wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.