Susan Mashibe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Suzan mashibe
Nchi Tanzania
Kazi yake uhandisi na urubani wa ndege

Suzan Mashibe (alizaliwa 1973) ni mkurugenzi na muasisi wa kampuni ya Tanjet, kampuni ya kimataifa na ya kwanza ya aina yake nchini Tanzania inayoshughulikia masuala ya kiufundi katika ndege binafsi, za biashara na hata za diplomasia[1].

Maisha yake[hariri | hariri chanzo]

Alipokuwa na umri wa miaka minne alitamani kuendesha ndege, na baadaye katika umri wa miaka 19 yeye alitoka nchini Tanzania akaenda kusoma marekani katika chuo cha Western Michigan.

Alipomaliza masomo yake alitunukiwa cheti cha FAA cha uhandisi na urubani wa ndege.[2] Ndiye mwanamke wa kwanza nchini Tanzania kutambulika na FAA kama mhandisi na rubani wa ndege.

Baada ya tukio la mfuatano wa mashambulizi manne yaliyotekelezwa na kundi la kigaidi la Al-Qaeda katika jengo maarufu la biashara (World Trade Center) nchini Marekani mnamo 11 Septemba 2001, Susan aliamua kurudi Tanzania na baadaye mwaka 2003 alianzisha kampuni iitwayo Tanjet ambayo kwa sasa inaitwa VIA.[3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Nakala iliyohifadhia". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-12-22. Iliwekwa mnamo 2018-09-12. 
  2. https://www.weforum.org/people/susan-mashibe
  3. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2018-10-18. Iliwekwa mnamo 2018-10-17. 
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Susan Mashibe kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.