Silabi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Silabi mwambatano)

Silabi ni kipashio cha kifonolojia kinachohusu matamshi ambapo sauti za lugha hutamkwa mara moja kwa pamoja kama fungu moja la sauti. Ama ni fungu la fonimu linalotamkika kwa pamoja na kwa mara moja. Kwa mfano katika neno kaka mna mafungu mawili: ka na ka.

Maneno kufanywa na silabi. Maneno mafupi huwa na silabi 1 pekee. Maneno mengine huwa na silabi zaidi kama 2, 3 au nyingi. Silabi fupi sana inaweza kuwa vokali 1 pekee au konsonanti 1 kama "m" katika "m-to-to".

Kama silabi inaishia kwa konsonanti inaweza kuitwa silabi iliyofungwa, kama inaishia kwa vokali inaweza kuitwa silabi wazi.

Kuna lugha zilizo na silabi nyingi zilizofungwa kama Kiingereza. Kiswahili kinapendelea silabi wazi, lakini "m" na "n" zinaweza kuwa mwishoni kwa silabi au kuwa silabi peke yake. Lugha kama Kijapani takriban hazina silabi za kufungwa.

Mifano ya maneno yenye silabi 1:

  • tu
  • na

Maneno mengi ya Kiswahili huwa na silabi mbili au zaidi:

  • ne-nda
  • ku-ja
  • shu-le
  • hi-i
  • ma-a-na
  • ra-fi-ki
  • se-ko-nda-ri
  • se-ri-ka-li
  • i-li-yo-fu-ngwa
  • m-to-to
  • m-ke
  • daf-ta-ri
  • lab-da

Kuna lugha zinazotumia mwandiko wa silabi badala ya alfabeti, kwa mfano abugida.

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Silabi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.