Sarafu ya Bit
Sarafu ya Bit (kwa Kiingereza: Bitcoin) ni mfumo wa malipo dijitali ambao unatumiwa na mamilioni ya watu bila msimamizi wa juu kama Benki Kuu ilivyo katika nchi mbalimbali. Sarafu hiyo huweza kutumika kwa kubadilishana na sarafu nyingine, bidhaa au huduma.
Sarafu ya Bit ilianzishwa na mtu asiyejulikana au kikundi cha watu chini ya jina la Satoshi Nakamoto [1] na kutolewa kama programu huria mwaka 2009. Kuanzia Februari 2015, wafanyabiashara zaidi ya 100,000 wanakubali Sarafu ya Bit kama malipo.
Kwa mujibu wa utafiti wa Chuo Kikuu cha Cambridge wa mwaka 2017, kuna watu kati ya milioni 2.9 hadi 5.8 wanaotumia malipo dijitali na wengi wao wanatumia sarafu ya bit. [2]
Mara nyingi sarafu ya bit inaitwa "pesa ya dijitali" lakini wataalamu wengi huiona si pesa bali bidhaa ya bahatisho. Paul Krugmann pamoja na wapokeaji wengine wa Tuzo ya Nobel ya Elimu ya Uchumi aliita udanganyifu [3] akiilinganisha na bahatisho la vitunguu vya maua ya tulip huko Uholanzi katika karne ya 17.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ "Who is Satoshi Nakamoto?", The Economist, The Economist Newspaper Limited, 2 November 2015. Retrieved on 23 September 2016. Archived from the original on 21 August 2016.
- ↑ Global Cryptocurrency Benchmarking Study. Jalada kutoka ya awali juu ya 2017-04-10. Iliwekwa mnamo 2017-10-16.
- ↑ Bubble, Bubble, Fraud and Trouble, Paul Krugmann katika New York Times tar. 29.01.2018, iliangaliwa Agosti 2018
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Mradi wa Sarafu ya Bit
- Video ya dakika tatu ikieleza maana ya sarafu ya bit
- Maelezo kuhusu Sarafu ya Bit imeelezwa kwenye tovuti ya Adam Rosen
- Blockchain Infographic Archived 9 Novemba 2020 at the Wayback Machine.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sarafu ya Bit kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |