Nenda kwa yaliyomo

Rafael Erich

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rafael Erich

Rafael Waldemar Erich (10 Juni 1879, Turku19 Februari 1946, Helsinki) alikuwa mwanasiasa wa Ufini kutoka Chama cha Kitaifa cha Muungano, Profesa, mwanadiplomasia, na Waziri Mkuu wa Ufini. Baraza la sita la mawaziri la Jamhuri ya Ufini, yaani baraza la mawaziri la Erich, lilidumu kuanzia 15 Machi 1920 hadi 9 Aprili 1921 kwa jumla ya siku 391.

Kazi na mafanikio makuu ya baraza la Erich yalikuwa ni mkataba wa amani na RSFR ya Urusi. Mkataba huo ulifanyika mjini Tartu, Estonia, tarehe 14 Oktoba 1920. Huu ndio ulikuwa wakati ambapo RSFR ya Urusi hatimaye ilitambua kikamilifu uhuru wa Ufini.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Rafael Erich kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.