Nenda kwa yaliyomo

Patricia Amira

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Patricia Amira ni mtetezi wa haki za wanawake na wasichana, mtangazaji, mzungumzaji wa hadhara na msimamizi wa mkutano wa Kenya, akitambuliwa kwa kipindi chake cha televisheni kilichotambuliwa kama The Patricia Show, ambacho kilitambulika Afrika kote, na pia Ulaya na Marekani, kuanzia 2009 hadi 2013.

Maisha ya Awali[hariri | hariri chanzo]

Amira alizaliwa Nairobi nchini Kenya. Alisoma Shule ya Kimataifa ya Geneva kati ya 1981 na 1985, na Chuo Kikuu cha Regent London kutoka 1989 hadi 1992.[1]

Tasnia ya habari[hariri | hariri chanzo]

Mnamo mwaka wa 2000 Amira alianza kufanya kazi kituo cha redio cha masafa ya 98.4 Capital FM, kituo cha pili cha redio huru kuanzishwa baada ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Kenya. Baadaye alihamia katika runinga, akiunda, kutayarisha na kusimamia kipindi cha The Patricia Show, ambacho kilirushwa Afrika, na pia huko Ulaya na Amerika, kati ya 2009 na 2013. Hivi karibuni, amewasilisha onyesho la saa 3 katika kipindi cha redio kilichotolewa kwa anuwai ya mitindo ya muziki ya Kiafrika.[2] [3] [4]

Ameonekana katika filamu moja iliyoitwa Rafiki, iliyooneshwa kwa mara ya kwanza katika Tamasha la Filamu la Cannes 2018, filamu ya kwanza ya Kenya kuonyeshwa kwenye tamasha hilo. Filamu hii ni hadithi ya mapenzi kati ya wasichana wawili katika shinikizo la familia na kisiasa nchini Kenya. Amira aliigiza kama mama wa mmoja wa wasichana hao.[5]

Utetezi wa haki za wanawake[hariri | hariri chanzo]

Amira ni mwenyekiti mwenza wa bodi ya Usawa ni sasa yaani Equality Now, (kwa lugha ya kiingereza) shirika lisilo la kiserikali la kimataifa lililoanzishwa mwaka 1992 ili kutetea ulinzi na uendelezaji wa haki za binadamu za wanawake na wasichana. Linafanya kazi ya kuhimiza serikali kupitisha, kuboresha na kutekeleza sheria zinazolinda na kukuza haki za wanawake na wasichana duniani kote, zikilenga katika kukomesha unyanyasaji wa kijinsia, kukomesha mila mbaya kama vile ndoa za utotoni na ukeketaji, kukomesha unyonyaji wa kijinsia ikiwa ni pamoja na biashara haramu ya kijinsia kwa wanawake na wasichana, na kukomesha ubaguzi wa kijinsia kisheria.[6]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Patricia Amira kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.