Nyoka Laini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyoka laini
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Colubridae (Nyoka walio na mnasaba na kipiri)
Oppel, 1811
Nusufamilia: Colubrinae (Nyoka wanaofanana na kipiri)
Oppel, 1811
Jenasi: Meizodon
Fischer, 1856
Ngazi za chini

Spishi 5:

Nyoka laini ni nyoka wa jenasi Meizodon katika familia Colubridae. Wamepewa jina hili kwa sababu ya ngozi yao laini.

Nyoka hawa ni wafupi na wembamba, sm 80 kwa kipeo lakini sm 30-60 kwa kawaida. Rangi ya wapevu ni kijivu au kahawia lakini nyoka laini kichwa-cheusi ni mwekundu au pinki wenye kichwa cheusi na shingo yenye mkufu mweusi. Wachanga ni kijivu au hudhurungi na kwa kawaida wana mabaka meusi angalau kichwani au kwa nusu ya mbele ya mwili pia.

Nyoka laini hukiakia mchana na hula mijusi, vyura na wagugunaji wadogo.

Nyoka hawa hawana sumu na wanaweza kukamatwa bila shida kwa sababu hawang'ati kwa kawaida.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyoka Laini kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.