Nebukadreza II

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tofali la kuchoma la Babuloni lenye jina na vyeo vya Nebukadreza.

Nebukadreza II (642 KK hivi – 7 Oktoba 562 KK) alikuwa mfalme bora wa Babeli katika karne ya 6 KK.

Alitawala sehemu kubwa ya Mashariki ya kati kuanzia Agosti 605 KK mpaka tarehe 7 Oktoba 562 KK.

Ni maarufu hasa kwa sababu aliwahi kuuvunja mji wa Yerusalemu mwaka 587 KK na kuwapeleka sehemu kubwa ya Wayahudi katika uhamisho wa Babeli.

Ndiye aliyejenga bustani za kupendeza katika enzi hizo zinazojulikana kama bustani za kuning'inia za Babeli, ambazo ni moja ya maajabu saba ya dunia.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

     . ISBN 978-1118455074
      . https://onlinelibrary.wiley.com/doi/abs/10.1002/9781118455074.wbeoe220.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nebukadreza II kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.