Nana Ama Dokua Asiamah Adjei

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nana Dokua Asiamah Adjei

Mbunge wa Ghana wa Akuapem Kaskazini Aliyepo madarakani
Amezaliwa 24 Julai 1982
Ghana
Nchi Ghana
Kazi yake mwanasiasa


Nana Dokua Asiamah Adjei (amezaliwa 24 Julai 1982) ni mwanasiasa wa Ghana na mbunge wa Jimbo la Akuapem Kaskazini Mashariki mwa Ghana. Ni mwanachama wa New Patriotic Party ambaye kwa sasa ni Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda wa Ghana. Hapo awali alikuwa Naibu Waziri wa Habari.[1][2][3][4]

Maisha ya utotoni na elimu[hariri | hariri chanzo]

Adjei alizaliwa tarehe 24 Julai 1982 na Nana Osae Nyampong IV na Aforo Asiamah-Adjei huko Akropong, Mkoa wa Mashariki. Alipata elimu yake ya msingi na shule ya upili katika Alsyd Academy na shule ya Upili ya St. Roses mtawalia. Ana shahada ya kwanza katika Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Ghana na shahada ya uzamili katika Logistiki na Ugavi kutoka Chuo Kikuu cha Exter nchini Uingereza.[5][6][1]

Maisha binafsi[hariri | hariri chanzo]

Adjei ameolewa na Charles Bissue. Kwa upande wa dini yeye amejitambulisha kuwa ni Mkristo.[6]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 "Election 2016: Know your female parliamentary candidates (4)". Graphic Online (kwa en-gb). Iliwekwa mnamo 2022-03-22. 
  2. "11 Young And Beautiful Ghanaian Female MPs Who Are Inspiring Girls To Dream Big". web.archive.org. 2018-10-25. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2018-10-25. Iliwekwa mnamo 2022-03-22. 
  3. "Nana Ama Dokua Asiamah Adjei", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2021-07-18, iliwekwa mnamo 2022-03-22 
  4. "Mahama is Africa’s “most incompetent election observer” – Ama Dokua". Citinewsroom - Comprehensive News in Ghana (kwa en-US). 2018-04-09. Iliwekwa mnamo 2022-03-22. 
  5. "Nana Ama Dokua Asiamah Adjei", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2021-07-18, iliwekwa mnamo 2022-03-22 
  6. 6.0 6.1 "MPs". Ghana MPS (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2022-03-22. 
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nana Ama Dokua Asiamah Adjei kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.