Monica Nashandi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Monica Nashandi (jina lingine Shivolo, alizaliwa tarehe 12 Oktoba 1959) ni mwanadiplomasia na mwanasiasa wa Namibia. Nashandi alikuwa balozi wa Namibia katika nchi za Skandinavia pamoja na alikuwa Mwakilishi wa Juu wa Uingereza. Nashandi aliondolewa kutoka kwenye orodha ya SWAPO kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2009 kwa sababu hakujiandikisha kupiga kura, kulingana na sheria za Namibia. Nashandi alikuwa balozi wa Namibia nchini Marekani kutoka mwaka 2019 hadi 2020.[1]


Maisha ya awali na elimu[hariri | hariri chanzo]

Nashandi alizaliwa tarehe 12 Oktoba 1959 katika kijiji cha Ompundja katika Mkoa wa Oshana. Kama mkimbizi mwaka 1978, alinusurika katika Vita vya Cassinga, shambulio la angani la Afrika Kusini dhidi ya SWAPO kwenye mpaka na Angola. Baadaye, alipata mafunzo ya kijeshi na kujiunga na Jeshi la Ukombozi la Watu wa Namibia (PLAN), mrengo wa kijeshi wa SWAPO wakati wa Vita vya Kupigania Uhuru wa Namibia.[2] Nashandi alihitimu nakupata diploma katika vijana na maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Zambia mwaka 1983 na alipata shahada ya uzamili katika masomo ya kidiplomasia kutoka Chuo Kikuu cha Westminster mwaka 2002 wakati akiwa kwenye majukumu ya kidiplomasia.


Kazi[hariri | hariri chanzo]

Baada ya uhuru wa Namibia mwaka 1990, Nashandi alihudumu kama Naibu Mkuu wa Itifaki katika Ikulu ya Namibia kabla ya uteuzi wake katika Wizara ya Mambo ya Nje kama Naibu Katibu Mkuu wa Masuala ya Kisiasa na Kiuchumi. Kuanzia mwaka 1995 hadi 1999, alikuwa balozi wa Namibia nchini Uswidi, Norwei, Denmark, Finland na Iceland. Kuanzia mwaka 1999 hadi 2005, alikuwa balozi wa nchi yake nchini Uingereza na Ireland.

Nashandi amekuwa mwenyekiti msaidizi asiye mtendaji wa bodi katika Trustco Group Holdings Limited tangu mwaka 2006. Trustco Group Holdings ni kampuni inayouza hisa hadharani ambayo hutoa bima ya mikopo midogo na huduma za kifedha.[3] Mnamo Novemba 2007, Nashandi aliteuliwa kuwa mwanachama wa bodi ya wakurugenzi wa Africon, kampuni ya uhandisi ya Namibia. Wakati wa uteuzi wake, alikuwa mwanamke pekee katika bodi.[4]


Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Tjitemisa, Kuzeeko. "Geingob reshuffles diplomatic pack", 11 December 2020. 
  2. Ndjebela, Toivo. "State House's Nashandi resigns", 16 October 2009. Archived from the original on 16 March 2012. 
  3. "Trustco Holdings". www.tgi.na (kwa en-GB). Iliwekwa mnamo 2017-09-08. 
  4. "Nashandi appointed to Africon board", 16 November 2007. 
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Monica Nashandi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.