Micere Githae Mugo
Micere Githae Mugo (alizaliwa Madeleine Micere Githae; 1942 - 2023) alikuwa mwandishi wa filamu na vitabu na mwanaharakati, muongozaji na mtunzi wa mashairi kutoka Kenya[1]. Alikuwa mhakiki wa kusoma na kuandika na Profesa wa kazi za Fasihi katika Kitengo cha mafunzo ya watu wenye asili ya Afrika katika chuo kikuu cha Syracuse, New York huko Marekani.
Maisha ya awali
[hariri | hariri chanzo]Mugo alizaliwa Baricho, wilaya ya Kirinyaga, mwaka 1942, akiwa mtoto wa walimu wawili waliokuwa wakishiriki siasa na kuhusika katika kupigania uhuru wa Kenya. Alisoma katika shule ya msingi na ya sekondari akiwa huko kenya na kusoma katika shule ya Alliance Girls kwenye ngazi ya kidato cha tano na sita[2]. Ndiye mwanafunzi wa kwanza Mweusi kusoma kwenye shule ambayo ilikuwa ikibagua mwanafunzi kwa rangi ya ngozi zao.[3] Kisha akaendelea na elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Makerere, na baadaye Chuo Kikuu cha New Brunswick nchini Canada ambapo alipata Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu mwaka 1973.[4]Baada ya kurudi Kenya, alifundisha katika Chuo Kikuu cha Nairobi na baadaye akawa mmoja wa wanawake wa kwanza kuwa Dean wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii nchini Kenya.[5]
Uhamisho na kazi nje ya nchi
[hariri | hariri chanzo]Kazi yake ya uanaharakati ilisababisha kukamatwa na kudhulumiwa, na hatimaye alilazimika kuondoka Kenya mwaka 1982 baada ya jaribio la mapinduzi dhidi ya serikali ya Moi. Alipokoseshwa uraia wa Kenya kwa muda, alipewa uraia wa Zimbabwe na baadaye akarejea Kenya tena katika miaka ya 1990.[4]
Baada ya uhamisho, aliendelea kufundisha na kuandika akiwa Marekani na Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Aliwahi kusema kuwa alikuwa “mtoto wa ulimwengu” kutokana na kuishi na kufanya kazi katika mabara mengi.[6]
Kazi na mchango wa kifasihi
[hariri | hariri chanzo]Mũgo aliandika vitabu na mashairi yanayojikita katika utamaduni wa Kiafrika, haki za binadamu na mtazamo wa kifeministi. Miongoni mwa kazi zake maarufu ni tamthilia aliyoandika pamoja na Ngũgĩ wa Thiong’o, The Trial of Dedan Kimathi.[7]
Alikuwa pia mhariri na mshauri katika miradi mbalimbali ya elimu na fasihi barani Afrika.
Kifo
[hariri | hariri chanzo]Mũgo alifariki tarehe 30 Juni 2023 huko Syracuse, New York akiwa na umri wa miaka 80 kutokana na saratani aliyokuwa akiishi nayo kwa muda mrefu.[8]
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Micere Mugo (Micere Githae Mugo) Biography - (1942– ), (Micere Githae Mugo), Visions of Africa, The Long Illness of Ex-Chief Kit, Disillusioned". www.jrank.org (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-02-17.
- ↑ "Alliance Girls High School:: Historical Perspectives". web.archive.org. 2011-09-03. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-09-03. Iliwekwa mnamo 2022-02-17.
- ↑ "Answers - The Most Trusted Place for Answering Life's Questions". Answers (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-02-17.
- 1 2 Douglas Killam, Ruth Rowe, mhr. (2000). The Companion to African Literatures. James Currey. ku. 166–167.
- ↑ "Senate Debates – Symposium in Honor of Prof. Micere Mugo" (PDF). Senate ya Kenya.
{{cite web}}: line feed character in|title=at position 7 (help) - ↑ "Micere Githae Mugo Biography". Answers.com.
{{cite web}}: line feed character in|title=at position 7 (help) - ↑ "SU Poet, Playwright, Activist Garners International Spotlight". Syracuse University News. 25 Machi 2013.
{{cite news}}: line feed character in|title=at position 3 (help) - ↑ "Distinguished Playwright & Poet, Micere Mugo Dies". Citizen Digital. 1 Julai 2023.
{{cite news}}: line feed character in|title=at position 14 (help)