Uchongaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mchongaji)
Mfalme Daudi alivyochongwa na Michelangelo katika marumaru labda ni sanamu maarufu zaidi duniani; iko katika Galleria dell'Accademia (Italia).
Uchongaji, sehemu ya kigae katika Campanile di Giotto huko Firenze (Italia).

Uchongaji ni aina mojawapo ya sanaa ambayo inatengeneza umbo la kupendeza kutokana na vitu rafu, kama vile mawe au mbao.

Sanaa hiyo ni ya zamani sana, lakini inazidi kuona njia mpya.

Uchongaji umekuwa wa msingi kwa tamaduni nyingi. Katika karne zilizopita sanamu kubwa za bei ghali ziliundwa kwa ajili ya watu binafsi, kwa kawaida zilikuwa mahususi kwa maonyesho ya dini au siasa.

Tamaduni hizo, ambazo sanamu zake zimesalia kwa wingi, ni pamoja na tamaduni za kale za Mediterania, India na Uchina, na pia nyingi za Amerika ya Kati na Kusini na Afrika.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: