Tanganyika African National Union : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d kurekebisha viungo vya makala zinazotofautisha maana
Mstari 11: Mstari 11:
[[de:Tanganyika African National Union]]
[[de:Tanganyika African National Union]]
[[en:Tanganyika African National Union]]
[[en:Tanganyika African National Union]]
[[it:Unione Nazionale Africana del Tanganica]]
[[nl:Tanganyika African National Union]]
[[nl:Tanganyika African National Union]]

Pitio la 14:31, 12 Aprili 2008

Tanganyika African National Union (TANU) kilikuwa chama kilichotawala Tanganyika na Tanzania hadi muungano wa chama hiki na Chama cha Afro-Shirazi cha Zanzibar ulipounda Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977.

TANU ilianzishwa Julai 7, 1954 kutokana na Tanganyika African Association (TAA). TAA ilikuwa na mwelekeo wa kitamaduni zaidi ya siasa. Mwenyekiti wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Kambarage Nyerere.

TANU ilishinda kila uchaguzi chini ya utawala wa kikoloni ikawa chama cha kuongoza Tanzania hadi ilipopata uhuru wake mwaka 1961. Katiba ya Taifa ya mwaka 1962 ilifanya TANU kuwa chama cha pekee nchini ikifuata mfano wa nchi za kijamaa zenye muundo wa siasa ya chama kimoja.