Larry Abramson

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Larry Abramson (2005).

Larry Abramson (1954) ni msanii kutoka nchi ya Israel.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Abramson alizaliwa mwaka 1954 katika Afrika Kusini mnamo mwaka wa 1961 [1], familia yake ilihamia Israel na kuanzisha makazi mjini Yerusalemu. Mnamo Mwaka wa 1970, kama mwandamizi katika shule ya sekondari, yeye alikuwa mmoja wa wale waliotia sahihi barua ya kupinga uvamizi wa kijeshi wa Gaza. Mwaka 1973, Abramson alikwenda kujifunza sanaa katika Chuo cha Chelsea ya Sanaa na ubunivu, London. Pindi tu aliporudi Israel yeye alichukua nafasi ya uchapishaji na mtunza ya maonyesho katika Warsha Print Yerusalemu, ambako alifanya kazi kwa miaka tisa, hadi 1986.

Maonyesho yake ya kwanza kibinafsi yalikuwa mwaka 1975. Kazi yake katika miaka ya 1980 yalishughulikia aina ya sanaa ya kisasa ishara kutoka Ulaya, hasa "Black Square" iliyoundwa na KAŽIMÍR Malevich, aliyoitumia kujenga hali ya nguvu kuchanganya mtindo wa kurahisisha na mfano wa sanaa ya kuchora.

Katika mwaka 1993 na 1994 Abramson aliunda mfululizo wa sanaa "Tsuba," iliyoonyeshwa katika Nyumba ya sanaa ya Kibbutz. Mfululizo huo ilijumuisha michoro asili 38 (mafuta kwenye turubai), michapisho 38 kwenye karatasi ya michoro ya asili, na picha za kisimama , kutokana na sampuli za mimea zilizochukuliwa kwenya maeneo. Mfululizo huu wa kazi inahusiana na magofu ya kiakeolojia iliyo karibu kibbutz Tzova, eneo ambayo ulitolewa muongo kabla yake na msanii Joseph Zaritsky (chini ya jina "Tsuba)." Wakati Zaritsky alipuuza magofu ya Waarabu yaliyopatikana kwenye eneo hilo kwa kulainisha uchoraji wake, Abramson alichora kihalisi. Kwa kujumuisha magofu ya kijiji Kiarabu, yeye alikosoa Zaritsky, ambaye inatakaali kutoa utambulisho wa Kiarabu kutoka kwenye eneo hilo.[2]

Mnamo Mwaka 1984, Abramson alijiunga na idara ya sanaa katika chuo cha Sanaa na ubunifu Bezaleli iliyoko Yerusalemu. Mwaka 1992, aliteuliwa mkuu wa idara ya sanaa na mkuu wa mipango Bezaleli kwa ajili ya wasanii chipukizi(shahada ya juu). Kwa mwaka wa masomo 2002-2003, yeye alialikwa kama mhadhiri mgeni na taasisi ya sanaa ya San Francisco; kwa wakati huo, huo alianza mchakato wa kuanzisha idara ya sanaa na ubunivu katika Chuo cha Uhandisi na ubunivu cha Shenkar katika eneo la Ramat Gan, Israel.

Mwezi tano 2002, Abramson alichapisha makala katika jarida Studio haki "We're all Felix Nussbaum," ambapo walijadili hali ya matatizo ya kujenga uchoraji wa kihistoria katika zama za baada ya ya mauaji ya wayahudi nchini ujerumani. Mnamo Mwaka 2004, Abramson aliweka maonyesho ya kazi chini ya jina "piles" kwa kutumia makaa. hii ilikuwa ni pamoja na michoro ya marundiko na uchafu ya ujenzi na yalikuwa yanahusiana na suala la magofu ikionyesha katika sanaa na sanamu ya mchoraji Felix Nussbaum wa Kijerumani aliyekuwa na asili ya Kiyahudi. Mfululizo huu iliwasilishwa katika Makavazi ya Felix Nussbaum katika Osnabrück, Ujerumani na katika makavazi ya Chaim Atar ya Sanaa katika kibbutz Ein Harod katika Bonde la Yezreeli.

Mnamo Mwaka 2007, Abramson aliwasilisha maonyesho ya uchoraji wake katika sanaa Gordon mjini Tel Aviv.

Tiniwayo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2015-01-05. Iliwekwa mnamo 2011-10-30.
  2. Levine, Angela (1998-11-06). Lessons in seeing. The Jerusalem Post. Iliwekwa mnamo 2011-09-20.

Gallery[hariri | hariri chanzo]