San Francisco

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mji wa San Francisco






Jiji la San Francisco

Bendera
Jiji la San Francisco is located in Marekani
Jiji la San Francisco
Jiji la San Francisco

Mahali pa mji wa San Francisco katika Marekani

Majiranukta: 37°46′46″N 122°25′09″W / 37.77944°N 122.41917°W / 37.77944; -122.41917
Nchi Marekani
Jimbo California
Wilaya San Francisco
Tovuti:  www.sfgov.org
Mahali pa San Fransisco katika Kalifornia
Reli ya manisipaa aina ya Cable Car
Bendera ya San Francisco

San Francisco ni mji wa Marekani uliopo kwenye mwambao wa Pasifiki katika jimbo la Kalifornia. Ni mji mkubwa wa nne wa Kalifornia ukiwa na wakazi 744,000.

San Francisco iko kwenye rasi kati ya Pasifiki na hori ya San Francisco. Mlangobahari wa kuingia katika hori huitwa "Golden Gate".

Mji hutembelewa na watalii wengi wanaopenda kuangalia daraja la Golden Gate, kisiwa cha Alcatraz na gereza lake, halafu kuzunguka mjini kwa reli za nyaya.

Mji unajulikana pia kwa jumuiya kubwa za mashoga na wabasha.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mji ulianzishwa na Wafransisko Wahispania mnamo 1776 kama sehemu ya koloni lao la Meksiko. Jina limechaguliwa kwa heshima ya mwanzilishi wao, Mt. Fransisko wa Asizi.

Baada ya vita vya Marekani dhidi ya Meksiko ya 1846 mji ukawa sehemu ya Marekani. Uchimbaji wa dhahabu ulisababisha ukuzi wa haraka.

Mwaka 1906 San Francisco iliharibiwa na tetemeko la ardhi ikajengwa upya.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu San Francisco kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.