Kuwekuwe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kuwekuwe
Kuwekuwe koo-jeupe
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Nicatoridae (Ndege walio na mnasaba na kuwekuwe)
Jenasi: Nicator
Hartlaub & Finsch, 1870
Ngazi za chini

Spishi 3:

Kuwekuwe ni ndege wadogo wa jenasi Nicator ambao wanatokea Afrika kusini kwa Sahara tu. Sikuhizi wataalamu wanaainisha ndege hawa katika familia yao Nicatoridae, lakini zamani walifikiri kuwekuwe ni aina za mbwigu (Laniidae) na baadaye wana wa familia Pycnonotidae.

Ndege hawa wanafanana na korogoto na wana rangi ya zaituni juu na nyeupe au kijivu chini. Wanatofautiana na korogoto kwa madoa meupe au njano mbawani. Chakula chao ni kama kile cha mbwigu: wadudu wakubwa na mijusi midogo. Tago lao hujengwa mtini na jike huyataga mayai 2-3.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]