Kurea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kurea
Kurea kidari-kijivu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Coraciiformes (Ndege kama viogajivu)
Familia: Alcedinidae (Ndege walio na mnasaba na midiria)
Nusufamilia: Halcyoninae (Ndege walio na mnasaba na kurea)
Jenasi: Actenoides Bonaparte, 1850

Caridonax Cabanis & Heine, 1860
Cittura Kaup, 1848
Clytocleyx Sharpe, 1880
Dacelo Leach, 1815
Halcyon Swainson, 1821
Lacedo Reichenbach, 1851
Melidora Lesson, 1830
Pelargopsis Gloger, 1841
Syma Lesson, 1827
Tanysiptera Vigors, 1825
Todiramphus Lesson, 1827

Kurea ni ndege wadogo wa nusufamilia Halcyoninae katika familia Alcedinidae. Spishi nyingine zinaitwa kichi au kijimbi-msitu. Wanafanana na midiria lakini ni wakubwa zaidi na spishi nyingi hutokea mbali na maji. Takriban spishi zote ni buluu mgongoni na domo lao ni jekundu mara nyingi. Spishi ndogo hula wadudu hasa lakini spishi kubwa zaidi hukamata kaa, vyura, mijusi, nyoka, panya au makinda ya ndege pia. Huchimba tundu katika ukingo wa mto, kichuguu au mti unaooza ambalo ndani lake jike huyataga mayai 2-5. Spishi nyingine zinatumia tundu la ndege mwingine kama zuwakulu au kigong'ota.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]