Kipwita

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kipwita
Kipwita mwekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Charadriiformes (Ndege kama vitwitwi)
Familia: Scolopacidae (Ndege walio na mnasaba na sululu)
Jenasi: Phalaropus
Brisson, 1760

Vipwita ni ndege wa jenasi Phalaropus katika familia ya Scolopacidae. Ndege hawa wana rangi ya nyeupe na kijivu. Wakati wa majiri ya kuzaa hupata rangi ya nyekundu angalau kwa ukosi wao (kipwita mwekundu ni mwekundu kwa mwili wote). Wanaweza kuogelea sana kwa sababu vidole vyao vina ndewe. Jike ana rangi kali kuliko dume na huanzisha ubembelezi. Dume huatamia na hutunza makinda. Mayai hutagwa tundrani kwa kanda za akitiki au mbugani kwa Amerika Kaskazini (Wilson’s phalarope). Nje ya majiri ya kuzaa hupisha wakati wao takriban wote kwa bahari kuu. Huonekana pia mara kwa mara kwa maziwa ya chumvi. Hula wadudu na gegereka.


Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi ya Amerika[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]