Tundra

Tundra ni eneo ambako miti haiwezi kustawi kutokana na halijoto duni na kipindi kifupi cha kuota kwa majani. Mara nyingi ardhi ya maeneo hayo iko katika hali ya jalidi ya kudumu yaani halijoto ya ardhi chini ya kina cha sentimita 30-200 ina halijoto chini ya sentigredi 0°C muda wote hata wakati wa "joto" katika maeneo hayo.
Kuna aina tatu za tundra:
Uoto wa mimea katika maeneo ya tundra ni hasa majani, kumvumwani na kuvu. Kama miti iko inatokea kwa umbo la vichaka vidogo. Mpaka kati ya maeneo ya tundra na maeneo ya misitu hujulikana kama "mstari wa miti".
Tabianchi katika maeneo ya tundra ni baridi kali na halijoto kidogo juu ya 0°C wakati wa wiki au miezi michache ya majira ya joto ilhali joto halitoshi kuyeyusha ardhi iliyoganda, isipokuwa kwenye sentimita za juu za ardhi.[1]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ English through Science (2010). Blue Planet. McGrawHill.
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Tundra kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |