Kipanga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa maana mengine ya jina hili angalia Kipanga (maana)

Kipanga
Kipanga wa Ulaya
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Accipitriformes (Ndege kama vipanga)
Familia: Accipitridae (Ndege walio na mnasaba na vipanga)
Nusufamilia: Accipitrinae (Ndege wanaofanana na vipanga)
Vieillot, 1816
Ngazi za chini

Jenasi 4:

Vipanga ni ndege mbua wa nusufamilia Accipitrinae katika familia Accipitridae. Ndege hawa ni wadogo kuliko tai na huruka upesi. Spishi nyingi zinatokea misituni na huwinda ndege na wanyama wadogo kwa kuruka haraka kutoka kitulio kilichofichwa. Wana mabawa mafupi na ya bapa, na mkia mrefu ili kuwasaidia kwenda huko na huko kati ya miti. Jike ni kubwa kulika dume. Uwezo wao wa kuona ni mzuri kabisa, mara nane ya uwezo wa binadamu.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]