Kiazeri-Kusini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kiazeri-Kusini ni lugha ya Kiturki nchini Azerbaijan, Uajemi, Uturuki, Iraq na Syria inayozungumzwa na Waazeri. Ni lugha tofauti na Kiazeri-Kaskazini ambayo ni lugha rasmi nchini Azerbaijan.

Mwaka wa 2010 idadi ya wasemaji wa Kiazeri-Kusini nchini Uajemi imehesabiwa kuwa watu zaidi ya milioni kumi na mbili. Pia kuna wasemaji milioni mbili nchini Iraq (2014), 248,000 nchini Azerbaijan, 540,000 nchini Uturuki (2014) na 44,000 nchini Syria (2014).

Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiazeri-Kusini iko katika kundi la Kiturki ya Kusini.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiazeri-Kusini kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.