Jupiter

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ukitafuta sayari inayoitwa Jupiter kwa lugha ya Kiingereza tazama Mshtarii
Sanamu ya Jupiter
Mkono wa sanamu ya Kiroma ya Jupiter unayoshika alama ya radi

Jupiter (pia: Iuppiter, Iovis) ni mkuu wa miungu katika dini ya Roma ya Kale. Analingana na Zeu katika dini ya Ugiriki ya Kale.

Kiasili Jupiter aliabudiwa kama mungu wa hali ya hewa aliyetawala radi na ngurumo. Baadaye alipewa nafasi ya baba wa miungu na pia wa wanadamu. Nembo yake ni radi anayoishika mkononi kwa sababu aliaminiwa ni mwenye uwezo wa kuzirusha.

Jupiter alikuwa na hekalu kubwa kabisa kwenye kilima cha Kapitoli mjini Roma penye mahekalu muhimu.

Katika utamaduni wa Kiroma sayari Mshtarii ilitazamiwa kama alama ya mungu huyu angani na sayari aliitwa kwa jina la Jupiter. Lugha nyingi za Kiulaya zinaendelea kutumia jina kwa sayari hii.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.