James Fraser Stoddart

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sir Fraser Stoddart mwaka 2016

James Fraser Stoddart (amezaliwa 24 Mei 1942) ni mwanakemia kutoka nchi ya Uskoti. Alifanya kazi katika Uskoti, Uingereza, Kanada na tangu mwaka 2002 Marekani. Hasa alichunguza jinsi molekuli kubwa zinaweza kuunganishwa kwa shabaha ya kuunda injini ya kimolekuli. Mwaka wa 2016, pamoja na Jean-Pierre Sauvage na Bernard Feringa alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia kwa michango yake ya kubuni na kuunda injini za kimolekuli[1][2][3] [4].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "for the design and synthesis of molecular machines"
  2. Staff. "The Nobel Prize in Chemistry 2016", Nobel Foundation, 5 October 2016. Retrieved on 5 October 2016. 
  3. "3 Makers of 'World's Smallest Machines' Awarded Nobel Prize in Chemistry", New York Times, 5 October 2016. Retrieved on 5 October 2016. 
  4. Davis, Nicola (5 October 2016). live. Iliwekwa mnamo 5 October 2016.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

5 Things to Know About ‘Molecular Machines’ , Time Magazine Oct. 5, 2016, iliangaliwa 23.10.2016

Makala hii kuhusu mshindi wa Tuzo ya Nobel bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu James Fraser Stoddart kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.