Indochina

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Indochina ya 1886

Indochina ni jina la kijiografia linalojumlisha maeneo ya kibara ya Asia ya Kusini-Mashariki (bila visiwa) upande wa kusini ya China na upande wa mashariki ya Uhindi.

Kihistoria ilitaja koloni ya Indochina ya Kifaransa iliyojumlisha maeneo ya nchi za

  • Kambodia
  • Laos
  • Vietnam

Mara nyingi pia maneeo ya

huhesabiwa kuwa sehemu za Indochina.

Kiutamaduni nchi hizi ziliathiriwa na Uhindi na China kwa viwango tofauti. Kwa jumla athira ya Uhindi ilikuwa kubwa lakini Vietnam imepokea mengi zaidi kutoka China.

Dini kuu ni Ubuddha hasa dhehebu ya Theravada. Ubuddha ya Mahayana iko zaidi Vietnam. Malaysia ina Waislamu wengi. Wahindu si wengi kwa sababu kihistoria Ubuddha ilichukua nafasi ya Uhindu.

Wakristo si wengi kwa jumla lakini makabila kadhaa yamepokea Ukristo kama sehemu za utamaduni wao.