Howard Wood (mwanamazingira)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Howard Wood OBE (alizaliwa 1954[1]) ni mwanamazingira wa Uskoti, mfadhili mwenza wa jumuiya ya Arran seabed Trust (COAST) na mshindi wa Tuzo ya mazingira ya Goldman mnamo mwaka 2015.[2]

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Howard Wood amekuwa akiishi kwenye Kisiwa cha Arran tangu akiwa na umri wa miaka 14, katika mji wa nyumbani kwa baba yake. Alifanya kazi katika kitalu cha miti, ambacho kilisimamiwa na familia yake. Tangu mnamo mwaka 1973 amekuwa akiogelea na kupiga mbizi katika bahari inayozunguka Kisiwa cha Arran. Ana ufahamu wa kina juu ya mazingira ya baharini. Wakati akichunguza mazingira ya baharini karibu na Kisiwa cha Arran, amechukua picha kadhaa na kuunda kumbukumbu za video.[1][2]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 "Archived copy". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-01-31. Iliwekwa mnamo 2016-08-20.  Unknown parameter |url-status= ignored (help)
  2. 2.0 2.1 "Howard Wood". Goldman Environmental Foundation. Iliwekwa mnamo 24 June 2021.  Check date values in: |accessdate= (help)