Ford Mustang
Ford Mustang ni gari la michezo maarufu sana la Marekani lililoundwa na kampuni ya Ford Motor tangu 1964.
Magari ya kwanza yalitengenezwa katika kiwanda cha Ford Dearborn, Michigan Machi 9 wa mwaka huo na gari lilionekana kwanza kwa umma tarehe 17 Aprili huko New York.
Halikugharimu pesa nyingi, lakini bado lilikuwa dhana sana na linaonekana kama gari kubwa zaidi. Watu wanaweza kuagiza magari haya kwa aina nyingi na kwa machaguo yao wenyewe.
Magari haya yanaweza kuokoa mafuta na kwenda kwa kasi. Zaidi ya milioni moja ya magari haya ya Mustang yalinunuliwa kwa miaka miwili tu.