Elimu Jamii Na Chemsha Bongo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Elimu Jamii Na Chemsha Bongo ni diwani ya mashairi iliyoandikwa na Charles Joseph Mloka ikiwa na mkusanyo wa mashairi ya aina nne: Elimu jamii, Siasa, Chemsha Bongo na Vituko [1]. Diwani hii ni toleo la pili la diwani ya kwanza iliyoitwa Elimu Jamii na Chemsha Bongo kwa Mashairi iliyotoka mwaka 2004 [2].

Katika kitabu hiki maudhui mbalimbali yameelezewa katika njia ya ushairi, ikiwemo elimu na walimu, kilimo na mapenzi, siasa, lakini mbali na hivyo yapo pia mashairi ambayo hayajaandikwa kwa lugha ya Kiswahili bali yametungwa katika lugha ya Kiluguru.

Kitabu hiki kimekusanya pia baadhi ya mashairi ya Kiingereza kutoka katika kitabu chake cha The Bush Rodent kilichotoka mwaka 2019 [3] na kuyatafsiri katika lugha ya Kiswahili.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. www.amazon.com https://www.amazon.com/ELIMU-JAMII-CHEMSHA-BONGO-Toleo-ebook/dp/B07VJCZVZ7. Iliwekwa mnamo 2020-02-10.  Missing or empty |title= (help)
  2. Mloka, Charles. (2004). Elimu jamii na chemsha bongo. Dar es Salaam: Mkukina Nyota Publishers. ISBN 9987-686-84-2. OCLC 123165263. 
  3. Mloka, Charles,. The bush rodent (toleo la Third edition). Milton Keynes. ISBN 978-1-7283-8731-4. OCLC 1099880955. 
Makala hii kuhusu kitabu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Elimu Jamii Na Chemsha Bongo kama Mwandishi wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.