Edwin Gyasi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Edwin Gyasi
Edwin Gyasi akiwa mazoezini

Edwin Gyasi (alizaliwa 1 Julai 1991 nchini Uholanzi) ni mchezaji wa soka wa Ghana ambaye sasa anacheza katika klabu ya Bulgaria CSKA Sofia na timu ya taifa ya Ghana.

Alicheza katika klabu mbalimbali kama vile Aalesund, Telstar, De Graafschap, FC Twente na Heracles Almelo.Yeye ni ndugu wa mchezaji wa soka anayeitwa Raymond Gyasi.

Kazi ya kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa huko Uholanzi lakini wazazi wake ni raia wa Ghana,Gyasi alicheza kwa mara yake ya kwanza katika timu ya taifa ya mpira wa miguu nchini Ghana katika ushindi wa kufuzu katika Kombe la Dunia la FIFA mwaka 2018 ambapo walishinda magoli 5-1 dhidi ya Kongo tarehe 5 Septemba 2017.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Edwin Gyasi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.