Dudumizi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Dudumizi
Dudumizi kichwa-cheusi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Cuculiformes (Ndege kama kekeo)
Familia: Cuculidae (Ndege walio na mnasaba na kekeo)
Nusufamilia: Centropodinae (Ndege wanaofanana na dudumizi)
Jenasi: Centropus
Illiger, 1811
Ngazi za chini

Spishi 29:

Dudumizi ni ndege wakubwa kadiri wa jenasi Centropus, jenasi pekee ya nusufamilia Centropodinae katika familia Cuculidae. Wana macho mekundu na mkia mrefu, na ukucha wa kidole kikabilicho nyuma ni mrefu sana. Jina “Centropus” linatoka maneno ya Kiyunani: κεντρον = mwiba na πους = mguu. Spishi nyingi zina mabawa kahawianyekundu na kichwa cheusi. Dudumizi hula wadudu, mijusi, nyoka na wanyama wadogo, na mayai, makinda, matunda na mizoga pia. Tago lao hujengwa katika uoto mzito na mara nyingi juu yake imefungwa. Jike hutaga mayai 2-5, lakini dume, ambaye ni mdogo zaidi, huatamia na hutunza makinda.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za Asia[hariri | hariri chanzo]

Spishi ya kabla ya historia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]