Dominik Szoboszlai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Dominik Szoboszlai

Nchi Uingereza
Kazi yake Mchezaji wa soka
Cheo mchezaji

Dominik Szoboszlai alizaliwa tarehe 25 Oktoba 2000, ni mchezaji wa soka kutoka Hungaria anayesakata dimba katika nafasi ya kiungo wa timu ya ligi kuu Uingereza ya Liverpool, na pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Hungaria.[1]

Akitokea kwenye timu ya vijana, Szoboszlai alifanya mwanzo wake wa kikosi cha wakubwa mwaka 2017 na klabu ya Austria ya FC Liefering, ambayo ni timu ya akiba ya Red Bull Salzburg. Januari 2018, Szoboszlai alianza kucheza katika klabu ya wakubwa, na kuwa mmoja wa wachezaji wa kwanza katika msimu wa 2018–19. Baada ya misimu mitatu, ambapo alisaidia klabu yake kushinda mataji matatu ya ligi na makombe ya ndani, Januari 2021, Szoboszlai alihamia Ujerumani kujiunga na RB Leipzig, klabu inayohusishwa na Red Bull Salzburg, kwa ada iliyoripotiwa kuwa €20 milioni, na kumfanya kuwa mchezaji wa Kihungaria mwenye thamani kubwa zaidi kuwahi kutokea. Katika misimu yake mitatu katika klabu hiyo, alisaidia timu yake kushinda mataji mawili ya DFB-Pokal. Julai 2023, alijiunga na Liverpool baada ya kulipa kifungu cha kuachiliwa cha €70 milioni, kumfanya kuwa usajili wa nne wenye gharama kubwa zaidi katika historia ya klabu hiyo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Price, Glenn (2 July 2023). "How do you pronounce 'Dominik Szoboszlai'? The man himself reveals". Liverpool FC. Iliwekwa mnamo 3 July 2023.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dominik Szoboszlai kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.