Madende

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Cichladusa)
Madende
Madende madoadoa Cichladusa guttata
Madende madoadoa
Cichladusa guttata
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Muscicapoidea (Ndege kama shore)
Familia: Muscicapidae (Ndege walio na mnasaba na shore)
Nusufamilia: Saxicolinae (Ndege wanaofanana na mihozo)
Vigors, 1825
Jenasi: Cichladusa
W. Peters, 1863
Ngazi za chini

Spishi 3:

Madende ni ndege wa jenasi Cichladusa katika familia ya Muscicapidae. Zamani waliainishwa katika familia ya mikesha (Turdidae). Wana mnasaba na kurumbiza na wanafanana nao. Wana rangi ya kahawa mgongoni na nyeupe chini; madende madoadoa ana madoa meusi kidarini na tumboni. Hawa ni ndege wa misitu mikavu ya Afrika. Madume ya spishi hizi waimba vizuri. Hula wadudu hasa. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika au chini ya kichaka. Jike huyataga mayai 2-4.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]