Kuchamwamba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Chaetops)
Kuchamwamba
Kuchamwamba kidari-chekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Corvoidea (Ndege kama kunguru)
Familia: Chaetopidae (Ndege walio na mnasaba na kuchamwamba)
Jenasi: Chaetops
Swainson, 1832
Spishi: C. aurantius E.L. Layard, 1867

C. frenatus (Temminck, 1826)

Kuchamwamba ni ndege wa jenasi Chaetops, jenasi pekee ya familia Chaetopidae, lakini spishi nyingine, kuchamwamba wa Damara, ni jamaa ya kucha wa Afrika. Spishi za Chaetops hazina mnasaba na kucha wengine bali na jamii ya kunguru.

Ndege hawa ni weusi wenye masharubu meupe na rangi ya machungwa au nyekundu kwa kidari, tumbo na kiuno. Mabawa yao ni mafupi kwa hivyo hawaruki angani sana lakini hukimbia na kurukia miwambani.

Wanatokea Afrika Kusini na Lesoto.

Hula wadudu hasa na mijusi, vyura, buibui, nge na nyungunyungu pia. Tago lao hujengwa kwa nyasi ardhini na jike hutaga mayai 2-3. Watoto wao wakubwa husaidia kutunza makinda.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]