Bubu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bubu akiwa amekaa.

Bubu (kwa Kiingereza: mute) ni mtu ambaye hana uwezo wa kusema au kuzungumza kwa kinywa kama ilivyo kawaida.

Mara nyingi watu hao huzungumza au kuongea kwa ishara tu. Kwa hiyo kama unataka kuongea na mabubu inabidi uweze kuzijua ishara zao wanazozitumia katika uzungumzaji na kutumia ishara hizo kwa umakini sana bila kukosea.

Mara nyingi hali hiyo ya ulemavu wa kimwili inawaathiri hata kinafsi. Hivyo si vyema kuwatenga au kuwanyanyasa watu kama hao maana wao ni binadamu wenzetu, inabidi tuishi nao kwa ushirikiano mkubwa na tusichoke kuwapa mahitaji yao jinsi inavyotakiwa.

Katika Injili, tunasoma Yesu alivyoponya baadhi ya mabubu, kama ilivyotabiriwa na manabii wa kale, hasa Isaya.

Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bubu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.