Wilaya ya Ilala
Wilaya ya Ilala ni wilaya moja ya Mkoa wa Dar es Salaam. Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 637,573 [1]. Eneo lake ni 273 km².
Ilala yenyewe inahesabiwa kama manispaa ya Ilala ndani ya jiji la Dar es Salaam. Inajumlisha kitovu cha kihistoria cha Dar es Salaam ambako kuna ofisi nyingi za serikali pamoja na makampuni makubwa na maduka. Nafasi ya kitovu chenyewe ni sanamu ya askari; mitaa mingine maarufu ni Kariakoo, Buguruni, Kivukoni na kando lake iko Pugu.
| Kata za Wilaya ya Ilala - Tanzania | ||
|---|---|---|
|
Buguruni • Chanika • Gerezani • Pugu • Msongola • Tabata • Kinyerezi • Ilala • Mchikichini • Vingunguti • Kipawa • Kariakoo • Jangwani • Kisutu • Mchafukoge • Ukonga • Upanga Mashariki • Upanga Magharibi • Kivukoni • Kiwalani • Segerea • Kitunda (Ilala) • |
||
| Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Ilala kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |