Wikipedia:Makala ya wiki/Joe Biden

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Joe Biden, Rais mteule wa Marekani

Joseph Robinette "Joe" Biden Jr. (amezaliwa 20 Novemba 1942) ni mwanasiasa wa Marekani.

Kuanzia mwaka wa 1973 hadi 2009 alikuwa mbunge wa Senati ya Marekani akiwakilisha jimbo la Delaware. Halafu alikuwa Makamu wa Rais wa Marekani chini ya Rais Barack Obama kuanzia mwaka wa 2009 hadi 2017, akiwa Mkatoliki wa kwanza na pia Mdelaware wa kwanza kuwa Kaimu Rais.

Mnamo Machi wa mwaka 2019, Biden alitangaza kugombea nafasi ya Rais wa Marekani mwaka 2020. Biden alishinda uchaguzi mkuu kwenye Novemba 2020 dhidi ya rais aliyetangulia Donald Trump. ►Soma zaidi