Siku ya Kimataifa ya Lugha ya Mama

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Shaheed Minar, au kumbukumbu la mashahidi, kwenye Chuo Kikuu cha Dhaka, Bangladesh, inayofanya ukumbusho wa wanafunzi waliokufa kwa ajili ya lugha ya Bangla tarehe 21 Februari 1952

Tarehe 21 Februari imetangazwa kuwa Siku ya Kimataifa ya Lugha ya Mama na UNESCO tarehe 17 Novemba 1999. Tangu tarehe ile imetambuliwa pia na Umoja wa Mataifa katika azimio lake la 16 Mei 2007, lililotangaza mwaka wa 2008 kuwa Mwaka wa Lugha wa Kimataifa.[1]

Asili ya Siku ya Lugha ya Mama ni tukio la mwaka wa 1952 nchini Bangladesh, wanafunzi wa chuo kikuu wa Dhaka walipofanya maandamano kwa ajili ya lugha ya Bangla, na wengine wao kuuawa na polisi kwa kupigwa risasi.

Siku ya Lugha ya Mama husherehekewa kila mwaka tangu mwaka wa 2000 na nchi zilizojiunga na UNESCO, kwa ajili ya kujadili mambo ya wingi wa lugha, haki za lugha zote, na mazingira ya kutumia lugha tofauti.

Yaliyomo

Mada za kila mwaka [hariri]

Kwa kawaida, Siku ya Lugha ya Mama ina mada tofauti kila mwaka.[2]

  • 2000, Sherehe ya kwanza
  • 2001, Sherehe ya pili
  • 2002, Wingi wa lugha: lugha elfu tatu ziko hatarini kufa
  • 2003, Sherehe ya nne
  • 2004, Elimu ya watoto[3])
  • 2005, Lugha kwa wasioona na kwa wasionena
  • 2006, Lugha na Mtandao
  • 2007, Elimu kwa lugha nyingi
  • 2008, Mwaka wa Lugha wa Kimataifa

Matukio mengine [hariri]

Marejeo [hariri]

Ona pia [hariri]

Viungo vya nje [hariri]

Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.