Shorobo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Shorobo
Shorobo domo-machungwa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Musophagiformes (Ndege kama shorobo)
Familia: Musophagidae (Ndege walio na mnasaba na shorobo)
Lesson, 1828
Ngazi za chini

Jenasi 5 na spishi 23:

Shorobo, dura au huruvi ni ndege wa familia Musophagidae. Spishi za jenasi Corythaixoides zinaitwa gowee pia na Tauraco fischeri anaitwa kulukulu. Spishi za jenasi Corythaixoides na Crinifer zina rangi ya kijivu na nyeupe, nyingine zina rangi ya majani, nyekundu, buluu na zambarau. Shorobo ni ndege wa pekee ambao wana pigmenti ya rangi ya majani inayoitwa turacoverdin. Ndege hawa wanatokea Afrika chini ya Sahara. Hawawezi kupuruka vizuri sana lakini hukimbia juu ya matawi ya miti. Hula matunda hasa na majani na maua pia, na mara chache hukamata wadudu na makoa. Hujenga tago lao kwa vijiti na jike hutaga mayai 2 au 3. Vinda wakitoka kwa mayai, wanapambwa na malaika mazito na macho yao ni wazi tayari au karibu.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]