Kodata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Chordate)
Kodata (Chordata)
Ugwe wa neva wa samaki huyu (Pristella tetra) uonekana kupitia ngozi
Ugwe wa neva wa samaki huyu (Pristella tetra) uonekana kupitia ngozi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Nusuhimaya: Eumetazoa
Faila ya juu: Deuterostoma (Wanyama ambao blastospori yao inakuwa mkungu)
Faila: Chordata
Kladi: Bilateria (Wanyama wenye uenzipacha)
Ngazi za chini

Nusufaila:':

Muundo wa kodata (samaki sahili): 1 = uvimbe wa ugwe wa neva ("ubongo"), 2 = notokodi, 3 = ugwe wa neva, 4 = mkia nyuma ya mkungu, 5 = mkungu, 6 = njia ya chakula, 7 = mfumo wa mzunguko, 8 = atriopori, 9 = uwanda kuzunguka koromeo, 10 = ufa wa tamvua, 11 = koromeo, 12 = uwanda wa mdomo, 13 = minyiri, 14 = mdomo, 15 = gonadi (ovari/kende), 16 = jicho sahili, 17 = neva, 18 = mkunjo wa tumbo, 19 = ini sahili

Kodata (kutoka lugha ya kisayansi: Chordata) ni kundi kubwa la wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni.

Ugwe unaunganisha neva ambazo ni muhimu kwa mwili kwa jumla na neva za kila sehemu au kiungo zinatoka hapa. Ugwe wa neva unaenda sambamba na mhimili wa seli ambazo ni imara zaidi ama gegedu au mfupa.

Mhimili huu ni chanzo cha uti wa mgongo kwa wanyama wengi wa kundi hili na kiunzi cha mifupa cha ndani ya mwili.

Kodata waliendelea kutoka kwa wanyama wengine kama Arthropoda wenye kiunzi cha nje.

Katika uainishaji wa kisayansi Kodata ni faila ya wanyama (Animalia). Nusufaila yenye spishi nyingi ni Vertebrata. Hapa mhimili wa kati unaendelea kuwa uti wa mgongo.

Samaki, amfibia, reptilia na mamalia ni oda ndani ya vertebrata.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kodata kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]