Omega
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Alfabeti ya Kigiriki | |||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Herufi za kawaida | |||||||
| Α α Alfa | 1 | Ν ν Ni | 50 | ||||
| Β β Beta | 2 | Ξ ξ Ksi | 60 | ||||
| Γ γ Gamma | 3 | Ο ο Omikron | 70 | ||||
| Δ δ Delta | 4 | Π π Pi | 80 | ||||
| Ε ε Epsilon | 5 | Ρ ρ Rho | 100 | ||||
| Ζ ζ Dzeta | 7 | Σ σ ς Sigma | 200 | ||||
| Η η Eta | 8 | Τ τ Tau | 300 | ||||
| Θ θ Theta | 9 | Υ υ Ipsilon | 400 | ||||
| Ι ι Iota | 10 | Φ φ Phi | 500 | ||||
| Κ κ Kappa | 20 | Χ χ Khi | 600 | ||||
| Λλ Lambda | 30 | Ψ ψ Psi | 700 | ||||
| Μ μ Mi | 40 | Ω ω Omega | 800 | ||||
| Herufi za kihistoria1 | |||||||
| 6 | 90 | ||||||
| 6 | 90 | ||||||
| 8 | 90 | ||||||
| 900 |
|
||||||
| 1 Viungo vya Nje: Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje |
|||||||
Omega ni herufi ya 24 pia ya mwisho katika alfabeti ya Kigiriki.
Jina la Kigiriki lamaanisha "O kubwa" kwa kutofautisha na Omikron au "O ndogo". Maana matamshi ya omega ilikuwa "o" ndefu.
Alama yake ilikuwa pia na maana ya namba 800.
Katika sayansi omega hutumiwa hasa kama alama ya omu (Ohm) yaani kipimo cha ukinzani wa umeme.
Omega ikiwa herufi ya mwisho ya alfabeti ya Kigiriki hutumiwa mara nyingi kwa kutaja mwisho. Hivyo ni kinyume cha mwanzo au alfa. Usemi wa Biblia hujulikana kuhusu Mungu kuwa ni "Alfa na Omega, mwanzo na mwisho" (Ufunuo wa Yohane 21:6).