Dzeta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kigiriki
Herufi za kawaida
Α α Alfa 1 Ν ν Ni 50
Β β Beta 2 Ξ ξ Ksi 60
Γ γ Gamma 3 Ο ο Omikron 70
Δ δ Delta 4 Π π Pi 80
Ε ε Epsilon 5 Ρ ρ Rho 100
Ζ ζ Dzeta 7 Σ σ ς Sigma 200
Η η Eta 8 Τ τ Tau 300
Θ θ Theta 9 Υ υ Ipsilon 400
Ι ι Iota 10 Φ φ Phi 500
Κ κ Kappa 20 Χ χ Khi 600
Λλ Lambda 30 Ψ ψ Psi 700
Μ μ Mi 40 Ω ω Omega 800
Herufi za kihistoria1
Digamma 6 San 90
Stigma 6 Sho 90
Heta 8 Koppa 90
Sampi 900
1 Viungo vya Nje:
Alfabeti_ya_Kigiriki#Viungo_vya_Nje

Dzeta (pia: Zeta) ni herufi ya sita katika Alfabeti ya Kigiriki. Inaandikwa kama ζ (alama ya kawaida) au Ζ (alama kubwa). Zamani za Kigiriki cha Kale ilikuwa pia tarakimu, ikiwa alama ya namba 7.

Asili ya dzeta ni herufi ya Kifinisia ya zayin (tazama makala ya herufi Z). Matamshi yake yalikuwa "dz", katika Kigiriki cha kisasa ni zaidi kama Z ya Kiswahili. Kutokana na herufi hiyo, alfabeti ya Kilatini ina "Z" na alfabeti ya Kikirili ina "З".

Jinsi ilivyo kawaida kwa herufi mbalimbali za Kigiriki ζ inatumiwa kama kifupisho kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hisabati na fizikia.