Mpito wa Zuhura

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Dunia, Jua na Zuhura wakati wa mpito wa Zuhura.
Mpito wa Zuhura kwenye mwaka 2004.
Msitari ya mpito wa Zuhura jinsi ilivyoonekana mwaka 1769 kwa mtazamaji huko Tahiti (nyekundu) na Vardø - Norwei (buluu). Kwa mtazamaji wa Tahiti Zuhura ilikuwa na njia fupi na kupita jua haraka zaidi. Tofauti kati ya vipimo mbalimbali iliruhusu kukadiria umbali wa Zuhura.

Mpito wa Zuhura mbele ya jua (kwa Kiingereza transit of Venus) unatokea wakati sayari Zuhura (Venus) inapita katika mstari baina ya jua na dunia.

Hii inalingana na kupatwa kwa jua kiasi. Ilihali Zuhura iko mbali inaonekana ndogo na kufunika sehemu ndogo ya jua tu kwa mtazamaji duniani.

Sayari ya Zuhura wakati huu inaonekana kama duara dogo jeusi linalopita polepole kwenye jua. Kwa kawaida mpito mmoja hudumu masaa kadhaa.

Mpito uliopita ulitokea mwaka 2012, na kabla yake mwaka 2004. Mipito ijayo itatokea Disemba 2117 na Disemba 2125. Mpito wa mwaka 2012 ulitazamwa na kurekodiwa kwenye intaneti.[1]

Mipito ya Zuhura inarudia kwa kufuata mfumo wa jozi mipito miwili kwa tofauti ya miaka minane; majozi hayo yana tofauti ya miaka 121.5 na miaka 105.5. Baada ya miaka 243 yote yanarudia.

Mtaalamu wa kwanza aliyetabiri mpito wa Zuhura kwa mwaka 1639 alikuwa Johannes Kepler lakini alifariki kabla ya tukio, hivyo hakuliona mwenyewe. Utabiri wake ulithibitishwa miaka 8 baadaye na Waingereza Jeremia Horrocks na William Crabtree wakati wa mpito wa pili tarehe 4 Disemba 1639.

Edmond Halley alitambua mwaka 1715 ya kwamba upimaji wa mpito wa Zuhura unaweza kuleta data za kuelewa umbali kati ya jua na dunia. Kutokana na makadirio yake jozi la mipito iliyofuata kwenye miaka 1761 na 1769 iliangaliwa na wanaastronomia wengi waliojiandaa na kusafiri kwenda maeneo tofauti ya dunia ili kupata vipimo vyenye nyuzi tofauti kati ya mtazamaji na jua. Safari mashuhuri ya nahodha na mpelelezi James Cook ilikuwa na lengo kuu kuwapeleka wanaastronomia hadi visiwa vya Tahiti kwa kutazama na kupima mpito huo.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. {http://www.exploratorium.edu/venus/ Webcast of the transit of Venus], tovuti ya exploratorium.edu. uliangaliwa Aprili 2017