Mkeshamsitu
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Mkeshamsitu | ||||||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mkeshamsitu kijani
(Cochoa viridis) |
||||||||||||||||||
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Mikeshamsitu ni ndege wa jenasi mbalimbali katika familia Turdidae. Spishi za Afrika zinafanana na chati na zina rangi ya kahawa mgongoni na nyeupe chini. Spishi za Asia zina rangi kali zaidi. Mwenendo wa ndege hawa ni kama ule wa mikesha. Wanatokea misitu ya majimaji ya Afrika na Asia, pengine milimani. Hula wadudu hasa na matunda pia. Hulijenga tago lao kwa vigoga, vijiti na mizizi katika mti. Jike huyataga mayai 3-5.
Spishi za Afrika [hariri]
- Alethe castanea, Mkeshamsitu Kishungi-chekundu (Fire-crested Alethe)
- Alethe diademata, Mkeshamsitu Mkia-mweupe (White-tailed Alethe)
- Pseudalethe choloensis, Mkeshamsitu wa Cholo (Thyolo Alethe)
- Pseudalethe fuelleborni, Mkeshamsitu Kidari-cheupe (White-chested Alethe)
- Pseudalethe poliocephala, Mkeshamsitu Kidari-kahawia (Brown-chested Alethe)
- Pseudalethe poliophrys, Mkeshamsitu Koo-jekundu (Red-throated Alethe)
Spishi za mabara mengine [hariri]
- Brachypteryx hyperythra (Rusty-bellied Shortwing)
- Brachypteryx leucophris (Lesser Shortwing)
- Brachypteryx montana (White-browed Shortwing)
- Chlamydochaera jefferyi (Fruithunter)
- Cochoa azurea (Javan Cochoa)
- Cochoa beccarii (Sumatran Cochoa)
- Cochoa purpurea (Purple Cochoa)
- Cochoa viridis (Green Cochoa)
- Heinrichia calligyna (Great Shortwing)
- Heteroxenicus stellatus (Gould's Shortwing)