Mkesha

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mkesha
Mkesha-mlima
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia: Turdidae (Ndege walio na mnasaba na mikesha)
Jenasi: Cataponera Hartert, 1896

Catharus Bonaparte, 1850
Chlamydochaera Sharpe, 1887
Cichlherminia Bonaparte, 1854
Cichlopsis Cabanis, 1850
Cochoa Hodgson, 1836
Entomodestes Stejneger, 1883
Geomalia Stresemann, 1931
Grandala Hodgson, 1843
Hylocichla S.F. Baird, 1864
Ixoreus Bonaparte, 1854
Myadestes Swainson, 1838
Neocossyphus Fischer & Reichenow, 1884
Nesocichla Gould, 1855
Platycichla S.F. Baird, 1864
Psophocichla Cabanis, 1860
Ridgwayia Stejneger, 1883
Sialia Swainson, 1827
Stizorhina Oberholser, 1899
Turdus Linnaeus, 1758
Zoothera Vigors, 1832

Mikesha ni ndege wa familia ya Turdidae ambao ni wadogo na wanono. Spishi za jenasi Neocossyphus na Stizorhina zinaitwa shesiafu pia. Rangi yao kuu ni rangi ya kahawia na madoa meupe na meusi; wengine wana rangi ya machungwa au nyekundu na wengine ni weusi. Hula wadudu hasa lakini wanaweza kula wanyama wadogo wengine, kama koa na nyungunyungu, na hata beri. Wengi wanaweza kuimba vizuri sana. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe na pengine hulawekea matope kwa ndani. Jike huyataga mayai 2-5 yenye vidoa.

[hariri] Spishi za Afrika

[hariri] Spishi za mabara mengine

[hariri] Picha