Lambo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Lambo la Aswan kwenye Ziwa la Nasser katika Misri
Ukuta wa lambo

Lambo ni bwawa au ziwa linalopatikana kwa kujenga ukuta unaozuia mwendo wa maji ya mto. Lambo laweza pia kukusanya maji ya mvua kwenye njia ya mtelemko wake.

Yaliyomo

[hariri] Shabaha ya kujenga lambo

Shabaha ya kujenga lambo ni hasa kupata akiba ya maji. Maji hutumiwa kwa ajili ya umwagiliaji, kama chanzo cha maji ya bomba kwa ajili ya watu au pia kwa utengenezaji wa umeme.

Lambo hujengwa pia kwa shabaha ya kuzuia mafuriko.

Malambo hujengwa mara nyingi katika mabonde ambako milima ya pande zote mbili inapunguza mahitaji ya kujenga ukuta mkubwa mno.

[hariri] Shida za malambo

Malabo yamekuwa pia na matatizo.

  • Ukuta unaathiri uwiano wa ekolojia kwa mfano lambo la Aswan linazuia matope yenye rutba kufika katika Misri
  • Umwagiliaji katika nchi za joto unaweza kuharibu ardhi ukiongeza chumvi katika ardhi kwa njia ya uvukizaji
  • Mara nyingi wenyeji asilia wamefukuzwa katika eneo la ziwa jipya bila kupewa makazi mazuri
  • Penye hatari ya tetemeko la ardhi uzani wa maji umeongeza matetemeko

[hariri] Malambo makubwa ya Afrika

Image:Karun3-dam.jpg

[hariri] Picha za malambo

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Lambo" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Lambo kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.