Ziwa la Nasser

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mahali pa Ziwa Nasser

Ziwa la Nasser (Kiarabu بحيرة ناصر buhairat nāssir) ni bwawa kubwa kwenye mto Nile iliyopatikana tangu kufungwa kwa mwendo wa Nile kwa lambo la Aswan nchini Misri kuanzia mwaka 1958.

Ziwa Nasser liko katika eneo la nchi za Misri na Sudan, hasa kati ya miji ya Aswan (Misri) na Wadi Halfa (Sudan). Eneo lake ni zaidi ya 5,200 km² lina urefu wa kilomita 550 na upana hadi 35 km. Mjao hufikia hadi 160 km³.

Jina lilitolewa kwa heshima ya aliyekuwa rais wa Misri Gamal Abdel Nasser aliyefanya azimio la kujenga bwawa.

[hariri] Faida na matatizo ya ziwa

Kuzuiliwa kwa mwendo wa mto ulimaliza mafuriko ya kila mwaka ya Nile nchini Misri. Kwan upande mwingine matope yenye rutba hayafiki tena chini ya Aswan na wakulima wahitaji kununua mbolea wa chumvi waliporidhika zamani na matope yaliyobaki mashambani baada ya mafuriko. Vilevile matope haya yameanza kujaza nafasi ya ziwa na mjao wake umeendelea kupungua polepole.

Pia delta ya Nile katika Mediteranea haikukua tena lakini imeanza kupungukiwa.