Uvukizaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Matone madogo madogo ya maji yaonekanavyo juu ya kikombe chenye chai ya moto
Matone ya mvuke wa maji kwenye sufuria

Uvukizaji (pia: mvukizo; ing. evaporation) katika fizikia ni mwendo wa kiowevu (majimaji) kugeuka gesi.

Kuna dutu kama maji zinazoanza kuvukiza kabla ya kufikia kiwango cha kuchemka. Viowevu vyote huvukiza vikifikia kiwango maalumu cha kuchemka.

Kama molekuli katika kiowevu zinapashwa moto mwendo wake unaongezeka. Zinagonganagongana na kuachana mbali zaidi hadi kuwa gesi.

Katika metorolojia uvukizaji ni hasa mwendo wa maji kuwa mvuke au gesi. Mwendo huu ni nguvu muhimu sana katika dura ya maji duniani. Maji ya baharini au unyevu nchini vinapashwa moto hasa na mionzi ya jua hadi kuwa mvuke unaopanda juu kuunda mawingu.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uvukizaji kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.